Machapisho

Inaonyesha machapisho yenye lebo ya Michezo

MAMELODI SUNDOWNS MABINGWA (CAF CHAMPIONS 2026)

Picha
Na,Thadeo Gelema   ​ Miamba ya soka kutoka Afrika Kusini, Mamelodi Sundowns (Bafana Ba Style), imetawazwa rasmi kuwa Mabingwa wapya wa Afrika baada ya kulazimisha sare ya 1-1 ugenini dhidi ya AS FAR Rabat ya Morocco katika mchezo wa pili wa Fainali ya CAF Champions League uliopigwa Jumapili, Mei 24, 2026, kwenye Uwanja wa Prince Moulay Abdellah jijini Rabat. ​ Kwa sare hiyo , Mamelodi Sundowns inayofundishwa na kocha Miguel Cardoso imetwaa ubingwa huo mkubwa zaidi ngazi ya klabu barani Afrika kwa ushindi wa jumla wa mabao 2-1 (aggregate), kufuatia ushindi wao wa bao 1-0 walioupata katika mchezo wa kwanza uliopigwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Loftus Versfeld jijini Pretoria. ​ Dakika 90 za Moto Jijini Rabat: ​Katika mchezo huo wa marudiano uliopigwa mbele ya umati mkubwa wa mashabiki wa Morocco, wenyeji AS FAR walikuwa wa kwanza kupata bao la uongozi mnamo dakika ya 40 kupitia mkwaju wa penati uliopigwa kwa usahihi na nahodha wao, Mohamed Hrimat, kufuatia faulu iliyofanywa ...

𝐀𝐑𝐒𝐄𝐍𝐀𝐋 𝐘𝐀𝐌𝐀𝐋𝐈𝐙𝐀 𝐊𝐈𝐁𝐀𝐁𝐄 𝐄𝐏𝐋, 𝐖𝐄𝐒𝐓 𝐇𝐀𝐌 𝐘𝐀𝐒𝐇𝐔𝐊𝐀 𝐃𝐀𝐑𝐀𝐉𝐀, 𝐆𝐔𝐀𝐑𝐃𝐈𝐎𝐋𝐀 𝐀𝐀𝐆𝐖𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐈𝐏𝐈𝐆𝐎

Picha
Na,Thadeo Gelema  Msimu wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) umefikia tamati leo Mei 24, 2026, kwa hisia mchanganyiko za furaha na simanzi baada ya kushuhudia mabingwa wapya wakiongeza nakshi kwenye taji lao huku miamba mingine ikishuka daraja rasmi.[1] ​ Ubingwa wa Arsenal Baada ya Miaka 22 Mabingwa wapya wa EPL, Arsenal FC, wamemaliza msimu kibabe kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 ugenini dhidi ya Crystal Palace katika Uwanja wa Selhurst Park jijini London.[1] Mabao ya washika mitandao hao wa London yalipachikwa na Gabriel Jesus pamoja na Noni Madueke, huku bao la kufutia machozi la Crystal Palace likifungwa na Jean-Philippe Mateta.[1 ] ​Licha ya kocha Mikel Arteta kufanya mabadiliko makubwa kwa kuwapumzisha nyota wake wengi wa kikosi cha kwanza, Arsenal bado ilionyesha soka safi na kuhitimisha msimu kwa furaha ya taji walilolisubiri kwa muda wa miaka 22.[1] ​ West Ham Washuka Daraja kwa Simanzi Upande wa pili, ulikuwa ni usiku wa majonzi makubwa kwa klabu ya West Ham United.[1] Licha ya...

𝐆𝐀𝐌𝐎𝐍𝐃𝐈; 𝐀𝐓𝐀𝐍𝐆𝐀𝐙𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐎𝐒𝐈 𝐂𝐇𝐀 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐒𝐓𝐀𝐑𝐒

Picha
Na,Thadeo Gelema    Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Miguel Gamondi, ametangaza rasmi kikosi cha wachezaji 24 watakaoingia kambini kujiandaa na michezo miwili ya kirafiki ya kalenda ya FIFA dhidi ya Uganda na Rwanda.[1] ​Macho ya mashabiki kote mikoani sasa yapo kwenye maandalizi haya ya kimkakati yatakayofanyika jijini Marrakesh, nchini Morocco, ambapo kikosi hicho kinatarajiwa kupimwa nguvu mapema mwezi Juni.[1] Taifa Stars itaanza kampeni yake kwa kucheza dhidi ya Uganda mnamo Juni 5, 2026, kabla ya kukipiga na Rwanda mnamo Juni 9, 2026.[1] ​ Orodha Kamili ya Wachezaji 24 Walioteuliwa: [1] ​Kikosi hiki kimebeba mchanganyiko wa kuvutia wa nyota wanaokipiga kwenye Ligi Kuu ya NBC (NBC Premier League) na wale wanaocheza soka la kulipwa katika klabu mbalimbali za nje ya nchi [1]: ​Makipa (Goalkeepers): ​Zuber Foba (Azam FC) [1] ​Aishi Manula (Azam FC) [1] ​Yona Amos (Pamba Jiji) [1] ​ Walinzi (Defenders): ​Pascal Msindo (Azam FC) [1] ​Nickson Kibabage (Sim...

𝐌𝐄𝐓𝐀𝐂𝐇𝐀; 𝐍𝐀𝐎𝐌𝐁𝐀 𝐑𝐀𝐃𝐇𝐈 𝐁𝐄𝐍𝐂𝐇𝐈 𝐋𝐀 𝐔𝐅𝐔𝐍𝐃𝐈 𝐍𝐀 𝐌𝐀𝐒𝐇𝐀𝐁𝐈𝐊𝐈

Picha
Na,  Thadeo Gelema  Golikipa wa Singida Black Stars, Metacha Mnata , ameomba radhi rasmi kwa viongozi, benchi la ufundi, na mashabiki wa klabu hiyo kufuatia sintofahamu iliyotokea katika mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Yanga SC uliochezwa Mei 22, 2026, kwenye Uwanja wa KMC Mwenge, jijini Dar es Salaam. ​Katika mchezo huo ambao Singida Black Stars ilikubali kichapo cha mabao 3-0, kulijitokeza picha ya kutoridhishwa na maamuzi ya benchi la ufundi wakati wa mchezo, jambo lililotafsiriwa kama utovu wa nidhamu. ​Kauli ya Metacha Mnata: ​Kupitia taarifa yake, Metacha amekiri kuwa kilichotokea kilitokana na mihemko na presha kubwa ya mchezo, lakini hakuwa na nia mbaya: "Klichotokea kilikuwa ni matokeo ya hisia za mchezo na presha ya ushindani, lakini haikuwa dhamira yangu kuonyesha utovu wa nidhamu wala kudharau maamuzi ya Benchi la Ufundi. Ninaiheshimu timu yangu, kocha wangu na maamuzi yote yanayofanywa kwa maslahi ya klabu." ​Ameongeza kuwa amejifunza kutokana na tukio hilo na an...

𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀 𝐘𝐀𝐕𝐔𝐍𝐉𝐈𝐊𝐀: 𝐀𝐋 𝐀𝐇𝐋𝐘 𝐊𝐎𝐌𝐁𝐄 𝐋𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈𝐒𝐇𝐎 𝐌𝐒𝐈𝐌𝐔 𝐔𝐉𝐀𝐎

Picha
Na,  Thadeo Gelema  Mizani ya soka nchini Misri imepinduka! Miamba ya soka barani Afrika, Klabu ya Al Ahly, itakosekana kwenye michuano ya CAF Champions League msimu ujao kwa mara ya kwanza kabisa ndani ya miaka 23, baada ya kumaliza nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu ya Misri. ​Waangukia Shirikisho ​Matokeo hayo yanaifanya Al Ahly kushuka na kushiriki Kombe la Shirikisho Afrika (CAF Confederation Cup) msimu ujao. ​Wakati Al Ahly wakiangukia huko, mahasimu wao wakubwa Zamalek wametwaa ubingwa wa ligi hiyo na kukata tiketi ya CAF Champions League, wakisindikizwa na Pyramids FC waliomaliza nafasi ya pili. ​ Historia ya Miaka 23 Yavunjika ​Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Capital Digital, mara ya mwisho kwa Al Ahly kukosekana kwenye michuano ya CAF Champions League ilikuwa ni mwaka 2003, kabla ya kuanza mfululizo wa kushiri michuano hiyo mikubwa ngazi ya klabu tangu msimu wa 2004. Kwa ujumla , Al Ahly kushuka hadi Kombe la Shirikisho baada ya miaka 23 ni pigo kubwa lin...

𝐀𝐑𝐒𝐄𝐍𝐀𝐋 𝐈𝐍𝐀 𝐒𝐔𝐁𝐈𝐑𝐈𝐀 𝐔𝐁𝐈𝐍𝐆𝐖𝐀 𝐋𝐄𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍 𝐂𝐈𝐓𝐘 ⚽🏆

Picha
Na, Thadeo Gelema  Manchester City leo inashuka dimbani kuivaa AFC Bournemouth katika mchezo muhimu wa Ligi Kuu England, huku City ikihitaji ushindi ili kuendelea kuweka presha kwa Arsenal kwenye mbio za ubingwa. Bournemouth wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na morali kubwa baada ya kufanya vizuri katika michezo yao ya nyumbani msimu huu, huku wakisaka nafasi ya kucheza michuano ya Ulaya kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo. Kwa upande wa Arsenal, wanakaribia kutwaa taji lao la kwanza la EPL baada ya miaka 22 tangu mafanikio ya kikosi cha “Invincibles” cha msimu wa 2003/04 kilichomaliza ligi bila kupoteza mchezo hata mmoja. Iwapo Manchester City watapoteza pointi katika mchezo wa leo, Arsenal watatangazwa rasmi mabingwa wa England. 🔥⚽

𝐔𝐖𝐀𝐍𝐉𝐀 𝐖𝐀 𝐉𝐀𝐌𝐇𝐔𝐑𝐈 𝐃𝐎𝐃𝐎𝐌𝐀 𝐖𝐀𝐅𝐔𝐍𝐆𝐈𝐖𝐀

Picha
Na, Thadeo Gelema    Leo 15, may 2026 Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeufungulia uwanja wa Jamhuri, Dodoma kutumika kwa michezo ya Ligi baada ya kufanya marekebisho yaliyokidhi vigezo vya kikanuni na sheria za mpira wa miguu. Uwanja huo uliofungiwa kutokana na miundombinu yake kutofaa kutumika kama ilivyoainishwa kwenye masharti ya Kanuni ya Leseni za Klabu umekaguliwa na kukidhi vigezo vya Kikanuni baada ya marekebisho yaliyoelekezwa kufanyika. Hata hivyo , TFF inaendelea kuzikumbusha klabu kuendelea kuboresha na kutunza miundombinu ya viwanja vyao vya nyumbani kwa kushirikiana na wamiliki kwa klabu ambazo hazimiliki viwanja, ili michezo ya Ligi ichezwe kwenye viwanja bora vinavyosaidia kuongeza ushindani na thamani ya Ligi. Kwa ujumla , Hatua hiyo ya TFF ni ishara ya kuendelea kuboresha mazingira ya mpira wa miguu nchini, huku ikisisitiza umuhimu wa viwanja bora katika kukuza ushindani, usalama wa wachezaji na maendeleo ya Ligi kwa ujumla.

𝐖𝐀𝐋𝐈𝐎 𝐌𝐂𝐇𝐎𝐊𝐀 𝐌𝐁𝐀𝐏𝐏É! 𝐙𝐀𝐈𝐃𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐈𝐋𝐈𝐎𝐍𝐈 30

Picha
Wimbi la mashabiki wanaotaka nyota wa Real Madrid, Kylian Mbapp é, kuondolewa ndani ya klabu hiyo limeendelea kuongezeka, huku zaidi ya watu milioni 30 wakidaiwa kusaini ombi hilo mtandaoni. Hatua hiyo imekuja kufuatia matokeo yasiyoridhisha ya hivi karibuni ya Real Madrid, ambapo taarifa zinaeleza kuwa timu hiyo imepata ushindi mmoja pekee katika mechi sita za mwisho alizocheza Mbappé. Aidha , baadhi ya wachambuzi wa soka wamebainisha kuwa Madrid imeonekana kufanya vizuri zaidi katika baadhi ya michezo ambayo mshambuliaji huyo hakuhusika. Hata hivyo , mjadala mkubwa umeendelea mtandaoni huku wadau wengine wakidai kuwa sehemu ya waliosaini ombi hilo huenda si mashabiki halisi wa Madrid, bali ni watu kutoka nje wanaochochea mjadala huo. 👉 Soma zaidi: @ thadeomedia5.blogspot.com

𝐓𝐈𝐌𝐔 𝐘𝐀𝐊𝐎 𝐈𝐍𝐀 𝐀𝐋𝐀𝐌𝐀 𝐍𝐆𝐀𝐏𝐈 𝐒𝐀𝐒𝐀? 🤔

Picha
Simba 🆚 Yanga = 2-2 ⚽ Hakuna mbabe leo 😮‍🔥 👉 Swali: Timu yako ina alama ngapi sasa? 🤔 Weka hapo chini 👇

DABI: WAAMUZI KUTOKA MOROCCO KUCHEZESHA

Picha
Na, Thadeo Media  Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara imewatangaza Waamuzi kutoka nchini Morocco, ambao wameteuliwa kwa ajili ya kuchezesha mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao utazikutanisha Simba na Yanga.Mwamuzi wa kati atakuwa Hamza El Fareq, na mwamuzi msaidizi Lahsene Agaou Uamuzi wa kuwaleta waamuzi wa kimataifa unaonesha dhamira ya kuhakikisha haki inatendeka uwanjani, hasa ukizingatia uzito wa pambano hilo ambalo huvuta hisia za mashabiki wengi ndani na nje ya nchi. Waamuzi hao wanakuja na uzoefu mkubwa wa kusimamia michezo ya kiwango cha juu, jambo linalotarajiwa kusaidia kudhibiti presha na kasi ya mchezo huo. Mchezo huo utakaopigwa kesho Mei 03, 2026 katika Uwanja wa Meja Isamuhyo unatarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku kila timu ikihitaji ushindi kwa malengo yake ya msimamo wa ligi.  Uwepo wa waamuzi hao kutoka Morocco unaongeza imani kwa wadau wa soka kuwa mchezo utaendeshwa kwa weledi, uwazi na kufuata sheria zote za mpira wa miguu, Hatua hiyo pia inaashiria ji...

𝐌𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄𝐊𝐈𝐓𝐈 𝐒𝐓𝐀𝐍𝐃 𝐔𝐍𝐈𝐓𝐄𝐃 𝐀𝐉𝐈𝐔𝐙𝐔𝐋𝐔 𝐆𝐇𝐀𝐅𝐋𝐀

Picha
Na Thadeo Gelema  Timu ya Stand United imeingia katika mabadiliko mapya ya kiuongozi baada ya Mwenyekiti wake wa mpito, Issa Mbaraka , kutangaza kujiuzulu rasmi wadhifa huo kufuatia changamoto za ndani zilizokuwa zikiikumba timu hiyo. Akizungumza na vyombo vya habari Mei Mosi, 2026 mkoani Shinyanga, Mbaraka amesema uamuzi wake umetokana na tofauti kubwa za kimtazamo kati yake na baadhi ya viongozi wenzake, hali iliyokuwa ikiathiri ufanisi wa majukumu yake pamoja na maendeleo ya timu. Ameeleza kuwa alichukua uamuzi huo kwa nia njema ya kuinusuru Stand United, ili kutoa nafasi kwa wengine kuendelea kuiongoza kwa mtazamo wanaouona unafaa zaidi. Mbaraka amesema aliteuliwa kushika nafasi hiyo mnamo Novemba 2025 na wadau wa timu, kwa lengo la kuirejesha katika ushindani mzuri baada ya kuwa katika kipindi kigumu cha matokeo yasiyoridhisha. Aidha , amebainisha kuwa licha ya jitihada zake za kuiboresha timu na kuanza kupata matokeo chanya, bado alikumbana na changamoto ya kukosekana k...

SERIKALI WAFANYA BIASHARA TUMIENI FURSA ZA AFCON 2027

Picha
  WAKATI hamu ya wapenzi wa soka barani Afrika ikielekezwa katika michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON 2027), Serikali ya Tanzania imetupa karata yake ya kwanza kwa sekta binafsi, ikitaka wafanyabiashara wa ndani kuwa mstari wa mbele kuchangamkia fursa zitakazotokana na mashindano hayo makubwa. Hatua hiyo imebainishwa kufuatia kikao muhimu cha Kamati Ndogo ya Maandalizi ya AFCON kilichofanyika jijini Dar es Salaam, kati ya Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma (Mwana FA), na uongozi wa Shirikisho la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wake, Deogratius Masawe. Tanzania, kwa mara ya kwanza katika historia, itakuwa mwenyeji wa mashindano hayo kwa ushirikiano na majirani zake Kenya na Uganda (Pamoja Bid). Kwa mujibu wa vyanzo kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), michuano ya AFCON imekuwa ikivuta watazamaji zaidi ya bilioni 1 duniani kote kupitia televisheni, huku maelfu ya mashabiki wakitarajiwa kumiminika nchini. Mhe...

MAPYA YAIBUKA MANGUNGU SIMBA KUANZA UTOAJI KADI ZA UANACHAMA MACHI 27, 2026

Picha
Hii ni Thadeo Media    Leo Februari 10, 2026   Klabu ya Simba SC imetangaza kuingia mkataba rasmi na kampuni za Mainstream Group na Nexus Pesa kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi la utoaji wa kadi mpya za uanachama, hatua inayolenga kuhuisha mfumo wa uanachama wa klabu hiyo kongwe nchini. Akizungumza kuhusu mpango huo, Makamu Mwenyekiti wa Bodi na Mwenyekiti wa Klabu ya Simba SC, Murtaza Mangungu, amesema kuwa utoaji wa kadi hizo utafanyika kwa kuzingatia kikamilifu katiba ya klabu, kuanzia ngazi ya matawi hadi makao makuu ya klabu. Mangungu amebainisha kuwa muda uliopo sasa ni muafaka hasa kwa wanachama waliopo kwenye matawi, huku akithibitisha kuwa zoezi la usajili wa matawi litaanza hivi karibuni kama sehemu ya maandalizi ya utoaji wa kadi hizo. “Klabu imepanga kuanza rasmi kutoa kadi za uanachama tarehe 27 Machi, 2026. Maandalizi haya yanahusisha taasisi mbalimbali, hivyo tumelazimika kuchukua muda ili kuhakikisha zoezi linafanyika kwa ufanisi na kwa kuzingatia taratibu...

CRISTIANO RONALDO AREJEA MAZOEZINI AL NASSR BAADA YA KUMALIZA MGOMO

Picha
Picha:Nyota wa Al Nassr na timu ya taifa ya Ureno, Cristiano Ronaldo. Picha na Mtandao Hii ni Thadeo Media   Nahodha wa Timu ya Taifa ya Ureno na nyota wa klabu ya Al Nassr, Cristiano Ronaldo, amehitimisha rasmi mgomo wake wa mechi kadhaa na kurejea katika mazoezi ya klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Saudi Arabia. Ronaldo alikuwa amekosa mechi mbili mfululizo baada ya kuibuka kwa sintofahamu ndani ya klabu hiyo, hali iliyotajwa kusababishwa na kutoridhishwa kwake na baadhi ya mambo ya kiuendeshaji yanayoendelea Al Nassr. Taarifa zinaeleza kuwa mchezaji huyo nguli alikerwa na changamoto za kifedha zinazoikumba klabu hiyo, hali ambayo imeathiri hata juhudi za usajili wa wachezaji wapya ili kuimarisha kikosi. Changamoto hizo zimedaiwa kusababisha sintofahamu kati ya uongozi wa klabu na baadhi ya wachezaji wakubwa. Aidha, Ronaldo pia alionesha kutoridhishwa na hatua ya hasimu wao mkubwa, Al Hilal, kumsajili mshambuliaji Karim Benzema, aliyewahi kuwa mchezaji mwenzake kwa miaka kadhaa...

ALLAN OKELLO: HADITHI YA NYOTA INAYONG’ARA KUTOKA LIRA HADI JANGWA

Picha
  Na,  Thadeo Gelema  Usiku wa Januari 12, saa 23: pazia lilifunguliwa. Young Africans SC waliandika sentensi mpya katika kitabu cha historia yao kwa kumtangaza Allan Okello, kiungo mshambuliaji mahiri kutoka Uganda. Haikuwa tu taarifa ya usajili, bali ilikuwa ni tangazo la matumaini mapya kwa Jangwani. Mzizi wa Safari: Alipozaliwa Ndoto Allan Okello alizaliwa Julai 4, 2000, katika mji wa Lira, kaskazini mwa Uganda. Ni eneo ambalo ndoto nyingi huanza bila viatu, lakini kwa mioyo mikubwa. Ndani ya mitaa ya Lira, Okello alianza kuizungumza lugha ya mpira mapema—pasi fupi, chenga tulivu na mguu wa kushoto uliojaa fikra. Akiwa bado kijana, kipaji chake kilimvuka umri wake. Ndiyo maana akaingia kwenye akademi za soka mapema kabla ya kuibuka rasmi katika ramani ya soka la Uganda. Kuzaliwa kwa Nyota: KCCA FC Mwaka 2017, akiwa na umri mdogo, Okello aliingia kwa kishindo katika klabu ya KCCA FC. Hapa ndipo jina lake lilipoanza kuandikwa kwa wino mzito katika soka la Uganda. Katika...

TAIFA STARS YAPATIWA KITITA CHA MILIONI 500 BAADA YA KUTINGA 16 BORA AFCON

Picha
Na,Thadeo Gelema  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameizawadia timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) shilingi milioni 500 kufuatia kufanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora katika michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON). Taarifa hiyo imetolewa leo Januari 03, 2026 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mwigulu Nchemba, wakati akizungumza na wachezaji pamoja na benchi la ufundi la Taifa Stars kwa njia ya simu. Waziri Mkuu Dkt. Nchemba amesema kuwa, Mheshimiwa Rais  amewapongeza wachezaji, benchi la ufundi pamoja na Watanzania wote kwa mafanikio hayo ya kihistoria na kusisitiza kuwa serikali itaendelea kuwaunga mkono timu hiyo. Aidha, Waziri Mkuu ameongeza kuwa, Rais Dkt. Samia ameahidi kutoa zawadi nono zaidi endapo Taifa Stars itaendelea kufanya vizuri na kufanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo inayoendelea nchini Morocco. 🇲🇦 Zawadi hiyo ya shilingi milioni 500 ni ishara ya kutambua na kuthamini jitihada za T...

Michezo

Picha
​"Taifa Stars vs Nigeria: Vita ya Daudi na Goliati Kwenye Ufunguzi wa Kundi C AFCON 2025"  Na, Thadeo Gelema  Mchezo wa Kundi C wa AFCON 2025 kati ya Nigeria 🇳🇬 na Tanzania 🇹🇿 bado haujaanza, lakini tayari umeanza kuvuta hisia za mashabiki wa soka barani Afrika. Huu ni mmoja wa michezo inayosubiriwa kwa hamasa kubwa, hasa kwa Watanzania wanaotamani kuona Taifa Stars ikiandika historia mpya. Historia ya Nigeria (Super Eagles) Nigeria ni miongoni mwa vigogo wa soka Afrika: Mabingwa wa AFCON mara 3 (1980, 1994, 2013) Wamefika fainali mara 6 Wamewahi kushiriki AFCON zaidi ya mara 19 Wanajulikana kwa wachezaji wenye nguvu, kasi na uzoefu mkubwa wa mashindano makubwa Kwa miaka mingi, Nigeria imekuwa ikipewa nafasi kubwa kwenye kila AFCON kutokana na rekodi na ubora wa kikosi. Historia ya Tanzania (Taifa Stars) Tanzania inaingia AFCON 2025 ikiwa kwenye safari ya kujitafuta upya: Ushiriki wa AFCON ni wachache ukilinganisha na Nigeria Haijawahi kuvuka hatua ya makundi Inaendelea k...

Michezo

Picha
  Je Unamjua👑Crown Prince Aliyezaliwa 2003 NDO ALIYE FUNGUA Rasmi AFCON 2025 Na, Thadeo Gelema  Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) yamefunguliwa rasmi usiku wa leo nchini Morocco, yakifunguliwa na Crown Prince wa Morocco, kijana aliyezaliwa mwaka 2003, hatua iliyovuta hisia za vyombo vya habari vingi vya ndani na nje ya nchi hiyo. Kwa mujibu wa ripoti kutoka vyombo mbalimbali vya habari vya Morocco, ikiwemo televisheni za kitaifa na majukwaa ya kidijitali, Crown Prince alihudhuria sherehe za ufunguzi zilizofanyika katika Uwanja wa Prince Moulay Abdellah, Rabat, akionyesha mshikamano wa kifalme na taifa katika tukio kubwa la michezo barani Afrika. Crown Prince huyo, ambaye ndiye mrithi wa ufalme wa Morocco, anatarajiwa kuwa Mfalme wa Morocco pindi Baba yake, Mfalme Mohammed VI, atakapong’atuka madarakani. Ushiriki wake katika ufunguzi wa AFCON umeonekana kama ishara ya kizazi kipya cha uongozi kinachothamini michezo, umoja wa Afrika na diplomasia ya kimataif...

Michezo

Picha
 Morali Juu! Paul Makonda Atua Morocco Kuipa Nguvu Taifa Stars Kuelekea Kibarua Kizito Dhidi ya Nigeria Na Thadeo Gelema  Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda amewasili nchini Morocco kwa lengo la kuipa nguvu na kuongeza morali kwa Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ya Wanaume Taifa Stars, inayoshiriki Michuano ya Mataifa ya Afrika AFCON 2025, nchini Morocco. Mhe. Makonda ameenda nchini Morocco kuiwakilisha Serikali katika kuwaunga mkono wachezaji na benchi la ufundi la Taifa Stars, ili kuhakikisha timu inapata hamasa na kujiamini kwenye michezo itakayoshindana.  Mara baada ya kuwasili, Mhe. Makonda alipokelewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Methusela Ntonda, akiambatana na Bw. Abel Philip, Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa wizara pamoja na Profesa Madundo Mtambo, Mjumbe wa kamati ya kitaifa ya maandalizi ya AFCON 2027.  Taifa Stars inatarajiwa kucheza mchezo wake wa kwanza tarehe 23 Desemba...

Michezo

Picha
  Morocco Yaichapa Comoros 2-0 Ufunguzi AFCON 2025 Na,Thadeo Gelema  Mchezo wa ufunguzi wa Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) umechezwa usiku wa Jumapili, Desemba 21, 2025, katika Uwanja wa Prince Moulay Abdellah, Rabat, ambapo Morocco iliibuka na ushindi wa mabao 2–0 dhidi ya Comoros. Morocco, ambao ni wenyeji wa mashindano haya ya 35, waliingia uwanjani wakiwa na presha kubwa ya mashabiki na rekodi zao nzuri za soka barani Afrika. Kwa mujibu wa viwango vya FIFA, Morocco inashika nafasi ya 11 duniani na namba moja Afrika, huku Comoros ikishika nafasi ya 108 duniani, jambo lililoifanya Morocco kuingia kama favorite. 📊 Matokeo ya Mwisho Morocco 2 – 0 Comoros 🇲🇦🇰🇲 ⚽ Brahim Díaz alifungua ukurasa wa mabao dakika ya 56, baada ya shambulio la kasi na mpangilio mzuri wa safu ya mbele ya Morocco. ⚽ Ayoub El Kaabi alihakikisha ushindi kwa bao la pili dakika ya 74, akifunga kwa shuti la kuvutia lililowasisimua mashabiki walioujaa uwanjani. Muhtasari wa Mchezo Li...