Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2026

𝐊𝐈𝐃𝐀𝐓𝐎 𝐂𝐇𝐀 𝐍𝐍𝐄 𝐀𝐅𝐀𝐑𝐈𝐊𝐈 𝐃𝐔𝐍𝐈𝐀 𝐒𝐇𝐈𝐍𝐘𝐀𝐍𝐆𝐀

Picha
  Shinyanga  Mwanafunzi wa kidato cha nne anayefahamika kwa jina la Rebecka Boniphace Maganga (1 7), aliyekuwa akisoma katika Shule ya Sekondari Old Shinyanga, amefariki dunia kwa tuhuma za kujinyonga ndani ya chumba alichokuwa akiishi. Tukio hilo lilitokea Aprili 27, 2026 majira ya saa saba mchana katika eneo la Old Shinyanga, ambapo inadaiwa mwanafunzi huyo alijinyonga kwa kutumia mkanda wa sketi ya shule. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi Janeth Magomi, jeshi la polisi lilipokea taarifa za tukio hilo kutoka kwa mlezi wa marehemu, Mashala Piter (56), ambaye aligundua tukio hilo. Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa tukio hilo linaweza kuhusishwa na msongo wa mawazo, baada ya mwanafunzi huyo kurejeshwa nyumbani na mwalimu wake akiwa na mzazi wake kufuatia kutohudhuria masomo kwa muda wa wiki mbili bila taarifa. Mwenyekiti wa kitongoji cha Senyenge , kijiji cha Old Shinyanga, Benjamin Andrew, alisema walipokea taarifa za tukio hilo maj...

𝐋𝐈𝐏𝐄𝐍𝐈 𝐓𝐎𝐙𝐎 𝐙𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐎𝐒𝐀 𝐁𝐀𝐑𝐀𝐁𝐀𝐑𝐀𝐍𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐓𝐈

Picha
Hii ni Thadeo Media  Madereva wa Magari Mkoani Shinyanga wamepatiwa elimu ya usalama barabarani kuhusu utii wa Sheria bila shuruti Kwa kulipa tozo zinazotokana na makosa ya usalama barabarani Kwa wakati ili kuepuka usumbufu wa kuzuiwa na kulipa madeni Kwa lazima pindi tozo hizo zinapokuwa zimeongezeka baada ya siku saba kuisha. Picha: inaonesha askari wa usalama barabarani akifanya ukaguzi kwa dereva wa gari la mizigo lililosimama pembeni ya barabara. Akitoa elimu hiyo Askari Polisi wa Kikosi Cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga Sajenti David Ndimila amewaelimisha madereva hao kuwa faida ya kulipa tozo hizo mapema inarahisisha usimamizi wa Sheria, inasaidia kuepuka usumbufu mara Kwa mara pia kuepuka adhabu Kali zaidi Picha: inaonesha askari wa usalama barabarani akiwa amesimama kando ya barabara akizungumza na dereva wa gari ndogo aina ya s Takix.  Aidha , Sajenti Ndimila amewataka wamikiki wa Magari kuwa na tabia ya kukagua Magari yao pindi wanapotoka kuwapa watu wengin...

SMAUJATA WAOKOA MTOTO WA MIAKA 10 MSALALA

Picha
Kahama, Shinyanga Kwa mjibu wa Misalaba media blog Katibu wa Jumuiya ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) Halmashauri ya Msalala , Bi. Nives Nyoni , aliiongoza operesheni ya kumwokoa mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 10 aliyedaiwa kufanyiwa ukatili na mama yake mzazi katika kijiji cha Isaka Station, wilayani Kahama mkoani Shinyanga. PICHA CHANZO: Misalaba Media Blog Tukio hilo lilitokea Aprili 23 , 2026 majira ya saa mbili usiku, ambapo mtoto huyo alikimbilia nyumbani kwa Bi. Nyoni kuomba msaada, akieleza kuwa alikuwa akipigwa mara kwa mara, alinyimwa haki ya kwenda shule na kufanyiwa vitendo vya mateso. Baada ya kupokea taarifa hiyo, Bi. Nyoni alimhifadhi mtoto huyo kwa muda na aliwasiliana na viongozi wa SMAUJATA, akiwemo Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga, Bi. Nabila Kisendi, kwa ajili ya hatua zaidi za uokoaji. Asubuhi iliyofuata , kwa kushirikiana na maafisa ustawi wa jamii wa Halmashauri ya Msalala pamoja na Jeshi la Polisi, mtoto huyo alipelekwa katika ...

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐑𝐔𝐊𝐈 𝐖𝐇𝐈𝐓𝐄 𝐇𝐎𝐔𝐒𝐄: 𝐌𝐀𝐔𝐀𝐉𝐈 𝐃𝐇𝐈𝐃𝐈 𝐘𝐀 𝐓𝐑𝐔𝐌𝐏

Picha
Hii ni Thadeo Media    Rais wa Marekani, Donald Trump, ameondolewa kwa haraka katika hafla ya White House Correspondents’ Dinner iliyofanyika jijini Washington, D.C., kufuatia tukio la taharuki lililosababishwa na milio inayodhaniwa kuwa ya risasi ndani ya ukumbi huo. Kwa mujibu wa taarifa za awali , Trump pamoja na viongozi wengine akiwemo Melania Trump na JD Vance walichukuliwa hatua za dharura na walinzi wenye silaha, huku wageni waliokuwapo wakijificha chini ya meza kutokana na hofu iliyozuka ghafla ukumbini. Ripoti za baadaye zinaeleza kuwa mshukiwa mmoja amekamatwa na yuko chini ya ulinzi wa vyombo vya usalama, huku uchunguzi ukiendelea kubaini chanzo halisi cha tukio hilo. Mamlaka zimeeleza kuwa hafla hiyo imesitishwa kwa muda ili kuruhusu uchunguzi wa kina kufanyika. Trump amethibitisha kuwa yeye pamoja na ujumbe wake wako salama, huku akiwahakikishia wafuasi wake kuwa hali iko chini ya udhibiti. Kwa ujumla , Tukio hilo limeibua taharuki kubwa na kuonesha umuhimu wa ...

KIMENUKA KAHAMA MTAJI LAKI 5, TOZO LAKI 3 NA 90! DC NKINDA HAJARIBIWI

Picha
Hii ni Thadeo Media,  Kahama Kwa mjibu wa malunde blog 1 Wafanyabiashara wa Soko la Namanga lililopo Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wameeleza kutoridhishwa na mfumo wa ukusanyaji wa ushuru wakidai kuwepo kwa tozo wanazoziita zisizo rasmi pamoja na ukosefu wa uwazi katika matumizi ya mapato yanayokusanywa sokoni hapo. Wakizungumza katika mkutano wa kusikiliza na kutatua kero ulioandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kahama katika soko hilo, wafanyabiashara wamesema wamekuwa wakikumbwa na mzigo mkubwa wa ushuru unaowadhoofisha kiuchumi, huku wakidai kuwa hakuna mrejesho wa wazi kuhusu matumizi ya fedha hizo. Mfanyabiashara wa samaki katika soko hilo Irene Thomas amesema kumekuwepo kwa vikundi vinavyohusika na ukusanyaji wa mapato ambavyo havitoi taarifa za kutosha kwa wafanyabiashara, hali inayozua sintofahamu sokoni hapo. "Sisi tunalipa ushuru zaidi ya maduka makubwa wanaolipa TRA, mimi mtaji wangu laki nne mpaka tano lakini kwa mwezi ushuru nalipa laki tatu na elfu tisini ni...

𝐃𝐂 𝐌𝐓𝐀𝐓𝐈𝐑𝐎 𝐌𝐀𝐑𝐔𝐅𝐔𝐊𝐔 𝐓𝐀𝐀𝐒𝐈𝐒𝐈 𝐙𝐀 𝐅𝐄𝐃𝐇𝐀 𝐊𝐔𝐅𝐈𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐌𝐀𝐋𝐈 𝐙𝐀 𝐖𝐀𝐍𝐀𝐍𝐂𝐇𝐈

Picha
Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akizungumza kwenye kikao kuangalia namna ya kumaliza changamoto ya taasisi za fedha zinazonyanyasa wananchi wanapochelewa kurejesha mikopo wanakwenda kuwafilisi mali zao jambo ambalo linakiuka sheria kwani wao hawana mamlaka hiyo. Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro ameanza kuchukuwa hatua kwa taasisi za fedha zinazokopesha fedha  kisha kwenda  kubeba vitu vya watu mtaani wanapokuwa wamechelewa kurejesha mikopo jambo ambalo ni kinyume cha sheria na taratibu. Hatua hiyo imechukuliwa kufuatia kuenea kwa mikopo umiza maarufu kama kausha damu, inayotolewa na baadhi ya taasisi na watu binafsi kwa riba kubwa, huku wakopaji wakikumbwa na vitisho na mali zao kuchukuliwa  wanaposhindwa kurejesha kwa wakati. Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro ametoa agizo wakati wa kikao na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za fedha,amesema vitendo vya kunyanyasa wananchi  havikubaliki na nilazima kuchukuwa hatua. Amesisitiza kuwa ni m...

"MIMI NI SAMIA YULE YULE "

Picha
Na mwandishi wetu, Dar Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa yeye ndiye yule yule na hajabadilika kama ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakidai kwenye Mitandao mbalimbali ya kijamii. Rais Samia amesisitiza hayo leo Alhamisi Aprili 23, 2026 Ikulu ya Magogoni Jijini Dar Es Salaam, akibainisha kuwa bado yeye ni Kiongozi anayeamini katika maridhiano kama ilivyokuwa falsafa yake tangu wakati amechukua uongozi wa Nchi. "Wakati nafuatilia uwasilishaji wa ripoti hii nilisikia sentensi inayosema 'Tunamtaka Samia wetu tunayemfahamu'- kanakwamba nilipoingia nilikuwa Samia mwingine na sasa ni Samia mwingine, nataka niwahakikishie watanzania kuwa mimi ni Samia yuleyule wa falsafa ya maridhiano (4R), ninachotaka ni ushirikiano wenu katika kutekeleza falsafa hiyo." Amesema Rais Samia. Rais Samia pia amewasihi watanzania kutokubali kurubuniwa na kuchochewa na wanaharakati, wanasiasa na wenye maslahi binafsi katika kuharibu tunu ya amani...

𝐂𝐇𝐄𝐓𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐙𝐈𝐑𝐈 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐁𝐀𝐑𝐈 𝐒𝐓𝐉𝐎𝐒𝐎 2𝐎25/26

Picha
Na, Thadeo Gelema  Katika hafla ya uapisho iliyofanyika Jumatatu, Aprili 13, 2026 chuoni hapo, viongozi mbalimbali walitunukiwa vyeti vya heshima kutokana na mchango wao katika uongozi na maendeleo ya wanafunzi. Miongoni mwa waliotunukiwa heshima hiyo ni Thadeo Gelema, aliyekuwa Waziri wa Habari STJOSO 2025/26, akitambuliwa kwa juhudi zake katika kukuza sekta ya habari ndani ya chuo hicho. Tuzo hiyo imeibua mjadala miongoni mwa wanafunzi na wadau wa habari, wakijiuliza iwapo hii ni ishara ya mwanzo mpya wa kuimarika kwa Thadeo haswa katika masuala ya habari 📲 Endelea kufuatilia na soma zaidi 👇👇 @thadeomedia5.blogspot.com

𝐂𝐇𝐔𝐊𝐔𝐄𝐍𝐈 𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐋𝐈 𝐊𝐖𝐄𝐍𝐘𝐄 𝐕𝐈𝐕𝐔𝐊𝐎 𝐕𝐘𝐀 𝐑𝐄𝐋𝐈

Picha
 Na, Thadeo Gelema  Maafisa usafirishaji maarufu kama bodaboda Manispaa ya Shinyanga wamepatiwa elimu ya usalama barabarani kuhusu kuheshimu vivuko vya reli ili kuepuka ajali za mara Kwa mara. Picha: Askari Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Sajenti David Ndimila, akitoa elimu kwa maafisa usafirishaji (bodaboda) kuhusu umuhimu wa kuheshimu vivuko vya reli. Elimu hiyo imetolewa na Askari Polisi wa Kikosi Cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga Sajenti David Ndimila katika kituo Cha Maafisa usafirishaji Cha Ally's star ambapo amewataka madereva hao kuheshimu vivuko vya reli Kwa kusimama na kujiridhisha hali ya kiusalama kabla ya kuchukua maamuzi ya kuvuka. Picha: Maafisa usafirishaji maarufu kama bodaboda wakimsikiliza kwa makini Sajenti David Ndimila wakati wa mafunzo ya usalama barabarani katika kituo cha Ally’s Star, Shinyanga. Sajenti Ndimila amewaelimisha kwamba Treni inapaswa kupewa kipaumbele kwahiyo kila mmoja anawajibika kuheshimu vivuko hivyo kuepukana na a...