Habari
HABARI PICHA: ZOEZI LA UCHANGIAJI DAMU CHUONI WALIVYO JITOKEZA KWA WINGI. picha ikionesha madaktari pamoja na wanafunzi wakiwa kwenye harakiti za zoezi lauchangiaji damu. Na: Thadeo Gelema SHINYANGA, Wanafunzi na watumishi wa chuo walijitokeza kwa wingi jana kushiriki mafunzo na zoezi maalumu la uchangiaji damu lililofanyika katika presentation room chuoni hapa. Zoezi hilo lilianza saa 4:00 asubuhi, likiwa na lengo la kuwahamasisha vijana na jamii kuhusu umuhimu wa kuchangia damu kwa hiari ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji damu hospitalini. Mhudumu wa afya akimpima mwanafunzi kama sehemu ya uchunguzi wa awali kabla ya zoezi Katika tukio hilo, wanafunzi waishio hostel na wale wa nje ya hostel walihudhuria kwa pamoja, wakionesha umoja na moyo wa kujitolea. Mwanafunzi akitoa damu kwa hiari, ishara ya moyo wa kujitolea miongoni mwa vijana wa chuo. Watumishi wa chuo nao walishiriki kwa hatua mbalimbali za maandalizi na uhamasishaji. Mmoja ya wanafunzi akifurahia ku...