Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2026

HAKUNA MGONJWA WA UVIKO-19 NCHINI – MHE. MCHENGERWA

Picha
Hii ni Thadeo Media – WAF, Dar es Salaam. Wizara ya Afya imewataka wananchi kuendela kuchukua tahadhari na kufuatilia ushauri wa kitaalam ili kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali kama ilivyoelezwa katika taarifa kwa umma ya Mganga Mkuu wa Serikali hivi karibuni. Hayo yamebainishwa leo Februari 27, 2026 Jijini Dar es salaam na Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa alipofanya ziara ya kimakakati katika hospitali ya Rufaa Mkoa Amana kwa lengo la kukagua utolewaji wa huduma za afya pamoja na maendeleo ya uboreshaji wa miundombinu ya hospitali hiyo. Aidha amesema, Serikali bado inaendelea kufuatilia kwa ukaribu juu ya mienendo ya magonjwa mbalimbali kama kipindu pindu, Dengue na UVIKO-19 hususani katika kipindi hiki cha mvua huku akisistiza kwamba hakuna kisa chochote UVIKO, cha mgonjwa aliyelazwa katika hospitali nchini. “Napenda kuwahakikishia wananchi na Watanzania wote Serikali yenu ipo makini na inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa maambukizi ya UVIKO-19 nchini na kimataifa,...

DC MTATIRO AENDESHA KLINIKI YA KERO SHINYANGA, MIGOGORO YA ARDHI YAONGOZA

Picha
Picha: Chanzo malunde 1 blog Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Wakili Julius Mtatiro akisikiliza kero za wananchi na migogoro Hii ni Thadeo Media Kliniki ya kusikiliza kero na migogoro ya wananchi imefanyika Wilayani Shinyanga kwa mafanikio makubwa, ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro. Kliniki hiyo imefanyika leo Februari 26,2026 katika eneo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya imelenga kuwapatia wananchi fursa ya kueleza changamoto zao moja kwa moja kwa uongozi wa serikali, pamoja na kutafuta suluhu za haraka na za kudumu. Wananchi wamejitokeza kwa wingi kushiriki kliniki hiyo, wakitoa kero mbalimbali zinazowakabili ambapo zaidi ya wananchi 200 wamejitokeza na kusikilizwa na mkuu wa Wilaya Mtatiro na wasaidizi wake. Ushiriki huo mkubwa umeonesha imani ya wananchi kwa serikali yao pamoja na utayari wa kushirikiana katika kutatua migogoro kwa njia ya amani na kisheria. Changamoto kubwa iliyojitokeza wakati wa kliniki hiyo ni uwepo wa migogoro mingi ya ardhi, ikiwemo mipaka ...

CHUKUA TAHADHALI KABLA YA KULIPITA GARI LINGINE

Picha
PICHA: Sajenti David Ndimila akitoa elimu ya usalama kwa madereva kuhusu namna sahihi ya kulipita gari barabarani .    Hii ni Thadeo media Leo February 26, 2026 Madereva wa magari makubwa yanayokwenda masafa marefu wamepatiwa elimu ya namna ya kujiepusha na ajali wanapotaka kuyapita magari mengine barabarani. Elimu hiyo imetolewa na Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga, Sajenti David Ndimila, ambaye amewataka madereva kujiridhisha kuwa hakuna hatari kwa watumiaji wengine wa barabara kabla ya kufanya uamuzi wa kulipita gari lililo mbele yao. Amesisitiza kuwa kabla ya kulipita gari la mbele, dereva anatakiwa kuacha nafasi ya kutosha kati ya gari analoliendesha na lile lililo mbele yake ili aweze kuona kwa urahisi magari yanayokuja kutoka upande wa mbele, na hivyo kufanya maamuzi sahihi na salama . PICHA: Mbali mbali Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga, Sajenti David Ndimila, akitoa elimu kwa madereva wa magari makubwa yanayosafiri masaf...

AZZA HILAL NAOMBA LAMI BARABARA YA DIDIA, TAA TINDE NA DIDIA

Picha
Picha: Chanzo: Malunde 1 Blog   Mbunge wa Jimbo la Itwangi, Mhe. Azza Hilal Hamad akizungumza katika kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Shinyanga. Picha: Chanzo: Malunde 1 Blog Mbunge wa Jimbo la Itwangi, Mhe. Azza Hilal Hamad akiwa kwenye kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Shinyanga. Na Thadeo Gelema Mbunge wa Jimbo la Itwangi, Azza Hilal Hamad, ameomba Serikali kuipandisha hadhi barabara ya Didia–Solwa ili iweze kuhudumiwa kwa kiwango kinachostahili kulingana na umuhimu wake kiuchumi na kijamii. Maombi hayo ameyatoa Februari 24, 2026 katika kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Shinyanga kilichohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa mkoa. Mhe. Azza amesema uboreshaji wa barabara hiyo utarahisisha usafirishaji wa mazao, kuimarisha upatikanaji wa huduma za kijamii na kufungua fursa zaidi za kiuchumi kwa wananchi wa Didia na Solwa. Sambamba na hilo, ameomba kuwekewa lami kipande cha barabara kutoka njiapanda ya Didia (Puni) hadi Didia Senta ili kuboresha miundombinu ya usafiri na kuchoche...

RASIMISHENI NAMBA ZA USAJILI ZA VYOMBO VYA MOTO.

Picha
Picha: Sajenti David Ndimila wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga akitoa elimu kwa dereva    Leo February 23, 2026 Madereva wa vyombo vya moto wametakiwa kufanya urasimishaji wa namba za usajili za vyombo hivyo pasipo shuruti mara baada ya kibali Cha muda mfupi kuisha. Akitoa elimu hiyo Kwa madereva wa vyombo vya moto Askari Polisi wa Kikosi Cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga Sajenti David Ndimila amewaeleza kuwa kuendesha vyombo vya moto Kwa kutumia namba ya chasi (chasiss number) bila namba ya usajili ni kosa kisheria mara baada ya muda wa kibali hicho Cha muda mfupi kuisha. Sajenti Ndimila amewataka madereva hao kujisimamia na kutekeleza takwa la kisheria bila shuruti pindi wanapotoa vyombo hivyo bandarini au kuvinunua vikiwa na namba ya chasi (chassis number) Picha: Sajenti David Ndimila wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga akitoa elimu kwa dereva, huku chombo cha moto kikiwa vimeegeshwa pembeni ya barabara wakati Mmiliki wake wakimsikili...

RAIS WA ST. JOSEPH COLLEGE ANGARA UZINDUZI WA JUKWAA LA VIJANA SHINYANGA

Picha
Picha inamuonyesha Vicent Chacha, Rais wa Chuo cha St. Joseph College Shinyanga, akiwa ameshere kwenye WhatsApp status yake leo, Februari 21, 2026, akionyesha ushirikiano wake na serikali na kuonyesha kuwa amewasilisha ombi la wanafunzi wa vyuo vya kati kuhusu mgawanyo sawa wa mikopo ya elimu .           Na Thadeo gelema Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo cha St. Joseph College Shinyanga, Vicent Chacha, ameitumia nafasi yake kuzungumza mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana kuwasilisha ombi la mgawanyo sawa wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya kati, akisisitiza kuwa nao ni Watanzania wenye haki ya kunufaika na fursa za kiuchumi. Vicent alisema kuwa mikopo hiyo itasaidia wanafunzi wa vyuo vya kati kumudu gharama za masomo na kujenga msingi imara wa maisha yao ya baadaye. Aliongeza kuwa kusikilizwa kwa hoja hiyo ni hatua kubwa kwa wanafunzi wengi waliokuwa wakikosa sauti ya kuwasilisha changamoto zao. Hatua hiyo imekuja sambamba na wito wa ...