𝐋𝐈𝐏𝐄𝐍𝐈 𝐓𝐎𝐙𝐎 𝐙𝐀 𝐌𝐀𝐊𝐎𝐒𝐀 𝐁𝐀𝐑𝐀𝐁𝐀𝐑𝐀𝐍𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐓𝐈

Hii ni Thadeo Media 

Madereva wa Magari Mkoani Shinyanga wamepatiwa elimu ya usalama barabarani kuhusu utii wa Sheria bila shuruti Kwa kulipa tozo zinazotokana na makosa ya usalama barabarani Kwa wakati ili kuepuka usumbufu wa kuzuiwa na kulipa madeni Kwa lazima pindi tozo hizo zinapokuwa zimeongezeka baada ya siku saba kuisha.

Picha: inaonesha askari wa usalama barabarani akifanya ukaguzi kwa dereva wa gari la mizigo lililosimama pembeni ya barabara.

Akitoa elimu hiyo Askari Polisi wa Kikosi Cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga Sajenti David Ndimila amewaelimisha madereva hao kuwa faida ya kulipa tozo hizo mapema inarahisisha usimamizi wa Sheria, inasaidia kuepuka usumbufu mara Kwa mara pia kuepuka adhabu Kali zaidi

Picha: inaonesha askari wa usalama barabarani akiwa amesimama kando ya barabara akizungumza na dereva wa gari ndogo aina ya s
Takix. 

Aidha, Sajenti Ndimila amewataka wamikiki wa Magari kuwa na tabia ya kukagua Magari yao pindi wanapotoka kuwapa watu wengine ili kujua kama yameandikiwa faini na kuweza kuwajurisha walioandikiwa faini wazilipe Kwa wakati.

Kwa ujumla, picha hizi zinaakisi operesheni ya usalama barabarani inayoendeshwa na Jeshi la Polisi mkoni Shinyanga 

🔚 Kwa ujumla, elimu iliyotolewa kwa madereva mkoani Shinyanga inaonesha umuhimu wa kuwajibika na kufuata sheria za usalama barabarani bila kulazimishwa. Ulipaji wa tozo kwa wakati si tu unasaidia kuepuka usumbufu na gharama za ziada, bali pia unachangia katika kuimarisha nidhamu ya matumizi ya barabara.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀