BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

DAR ES SALAAM: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa Wenyeviti wa Bodi katika taasisi mbalimbali za umma nchini.

Na, Thadeo Gelema 

​Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa leo Ijumaa, Mei 22, 2026, na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo unajumuisha viongozi wafuatao waliopangiwa

 kusimamia bodi hizo muhimu:

Orodha ya Walioteuliwa na Taasisi Zao:

Ludovick James Nduhiye – Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Kumbukumbu na Nyaraka za Taifa.


Dkt. Irene Charles Isaka – Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).


Jamhuri Joseph Ngelime – Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

kwa ujumla, Ufanisi Katika Utendaji

​Kwa mujibu wa taarifa iliyoripotiwa na Millard Ayo UPDATES, uteuzi huu wa viongozi unatarajiwa kuongeza kasi ya kiutendaji, uwajibikaji, pamoja na kuboresha mifumo ya usimamizi katika taasisi hizo za kimkakati kwa maendeleo ya nchi.



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀