𝐀𝐑𝐒𝐄𝐍𝐀𝐋 𝐈𝐍𝐀 𝐒𝐔𝐁𝐈𝐑𝐈𝐀 𝐔𝐁𝐈𝐍𝐆𝐖𝐀 𝐋𝐄𝐎 𝐊𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐍 𝐂𝐈𝐓𝐘 ⚽🏆
Na, Thadeo Gelema
Manchester City leo inashuka dimbani kuivaa AFC Bournemouth katika mchezo muhimu wa Ligi Kuu England, huku City ikihitaji ushindi ili kuendelea kuweka presha kwa Arsenal kwenye mbio za ubingwa.
Bournemouth wanaingia kwenye mchezo huo wakiwa na morali kubwa baada ya kufanya vizuri katika michezo yao ya nyumbani msimu huu, huku wakisaka nafasi ya kucheza michuano ya Ulaya kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo.
Kwa upande wa Arsenal, wanakaribia kutwaa taji lao la kwanza la EPL baada ya miaka 22 tangu mafanikio ya kikosi cha “Invincibles” cha msimu wa 2003/04 kilichomaliza ligi bila kupoteza mchezo hata mmoja.
Iwapo Manchester City watapoteza pointi katika mchezo wa leo, Arsenal watatangazwa rasmi mabingwa wa England. 🔥⚽

Maoni
Chapisha Maoni