DABI: WAAMUZI KUTOKA MOROCCO KUCHEZESHA
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara imewatangaza Waamuzi kutoka nchini Morocco, ambao wameteuliwa kwa ajili ya kuchezesha mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao utazikutanisha Simba na Yanga.Mwamuzi wa kati atakuwa Hamza El Fareq, na mwamuzi msaidizi Lahsene Agaou
Uamuzi wa kuwaleta waamuzi wa kimataifa unaonesha dhamira ya kuhakikisha haki inatendeka uwanjani, hasa ukizingatia uzito wa pambano hilo ambalo huvuta hisia za mashabiki wengi ndani na nje ya nchi.
Waamuzi hao wanakuja na uzoefu mkubwa wa kusimamia michezo ya kiwango cha juu, jambo linalotarajiwa kusaidia kudhibiti presha na kasi ya mchezo huo.
Mchezo huo utakaopigwa kesho Mei 03, 2026 katika Uwanja wa Meja Isamuhyo unatarajiwa kuwa na ushindani mkali, huku kila timu ikihitaji ushindi kwa malengo yake ya msimamo wa ligi.
Uwepo wa waamuzi hao kutoka Morocco unaongeza imani kwa wadau wa soka kuwa mchezo utaendeshwa kwa weledi, uwazi na kufuata sheria zote za mpira wa miguu, Hatua hiyo pia inaashiria jitihada za kuboresha ubora wa ligi na kuifanya iweze kushindana kimataifa.

Maoni
Chapisha Maoni