Na Mwandishi Wetu mbungeni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima amesema wizara hiyo ilipokea jumla ya mashauri 49,573 ya ndoa katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026. Akizungumza leo Juni 1, 2026 Bungeni, Jijini Dodoma wakati akiwasilisha Hotuba ya mapitio ya utekelezaji wa mpango wa bajeti ya mwaka 2025/2026 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2026/2027, Dkt. Gwajima amesema: “Katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026, Wizara kwa kushirikiana na OWM–TAMISEMI ilipokea mashauri 49,573 ya ndoa.” Pia Waziri Gwajima amefafanua kuwa kati ya mashauri hayo, 9,995 yalisuluhishwa na kufungwa na 8,036 yalipelekwa Mahakamani, huku 31,542 yakiendelea kusuluhishwa. Kwa ujumla, Takwimu hizi zinaweza kuonesha picha ya jamii inayokabiliwa na mabadiliko ya kijamii, ambapo migogoro ya ndoa inaongezeka kutokana na sababu mbalimbali kama uchumi, mawasiliano duni na changamoto za malezi .