MOTO WATEKETEZA STUDIO ZA BARNABA CLASSIC
Studio za mwanamuziki wa Tanzania, Elias Barnabas maarufu kama Barnaba Classic, zimeteketea kwa moto usiku wa kuamkia Juni 1, 2026 katika eneo la Mwananyamala jijini Dar es Salaam.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Barnaba amesema moto huo ulianza majira ya saa 2:30 usiku muda mfupi baada ya kutoka kwenye shughuli zake za kikazi. Amesema studio hizo zilikuwa zimefanyiwa ukarabati mkubwa wiki chache zilizopita kwa gharama kubwa.
Barnaba ameeleza kuwa tukio hilo limemuumiza kwa kuwa studio hizo zilikuwa zikitoa ajira na fursa kwa vijana wengi kupitia shughuli za muziki na uzalishaji wa kazi za sanaa.
Kwa ujumla, Pamoja na hasara iliyotokea, msanii huyo amesema anamshukuru Mungu kwa uhai na kuahidi kuanza upya huku akichukulia tukio hilo kama funzo la maisha.

Maoni
Chapisha Maoni