Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Breaking : UMMY MWALIMU MSHAURI WA RAIS SAMIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemteua Bi. Ummy Ally Mwalimu kuwa Mshauri wa Rais anayeshughulikia Masuala ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo umetangazwa leo Juni 2, 2026 kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Bi. Ummy Mwalimu ni mmoja wa viongozi wenye uzoefu mkubwa katika utumishi wa umma nchini, akiwa amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uwaziri katika Serikali ya Tanzania. Katika kipindi cha uongozi wake, amewahi kuhudumu katika sekta za afya, mazingira, Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐉𝐄, 𝐖𝐀𝐉𝐔𝐀? 𝐋𝐈𝐌𝐀𝐎 𝐍𝐈 𝐓𝐔𝐍𝐃𝐀 𝐀𝐔 𝐊𝐈𝐔𝐍𝐆𝐎!

𝐆𝐀𝐌𝐎𝐍𝐃𝐈; 𝐀𝐓𝐀𝐍𝐆𝐀𝐙𝐀 𝐊𝐈𝐊𝐎𝐒𝐈 𝐂𝐇𝐀 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐒𝐓𝐀𝐑𝐒