TOENI TAARIFA VITENDO VYA UKATILI SAFARINI

Abiria wa masafa marefu wamepatiwa elimu kuhusu kupaza sauti zao pindi wafanyiwapo au waonapo vitendo vya ukatili wa kijinsia vikitendeka ndani ya gari wawapo safarini
Picha: Abiria wakikumbushwa umuhimu wa kuheshimiana, kulinda mipaka ya mwili na kutoa taarifa mapema pindi wanapoona au kufanyiwa ukatili.
Akitoa elimu hiyo Askari Polisi wa Kikosi Cha usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga Sajenti David Ndimila amewataka abiria kutokukubaliana na vitendo hivyo kufanyika wakiwa safarini kama utolewaji wa lugha za udhalilishaji, kushikwa maungo  wanawake Kwa kisingizio Cha msongamano wa watu ndani ya gari, kupakatwa Kwa wanafunzi wa kike Kwa kisingizio Cha kukosa siti au kumdhalilisha mtu kulingana na umbo lake pia utolewaji wa lugha za vitisho.

Picha: Abiria wa safari ndefu wakisikiliza elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia wakielekezwa na askari polisi.
Aidha Sajenti Ndimila amewaeleza abiria kuwa mwili wa kila mtu ni wake, hakuna mtu mwenye haki ya kuugusa, kuuzungumzia au kumtumia kingono bila ruhusa yake kamili.

Picha: Sajenti wa usalama barabarani akizungumza na abiria kuhusu haki zao na umuhimu wa kuripoti vitendo vya ukatili.

Abiria wamesisitizwa kuwa kila mmoja awe mlinzi wa mwenzie Kwa kupaza sauti zao na kuzuia vitendo hivyo Kwa kutoa taarifa kwenye mamlaka husika ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Picha: Abiria wakihamasishwa kuwa walinzi wa wenzao kwa kupaza sauti na kutoa taarifa dhidi ya ukatili wa kijinsia.


Kwa ujumla, elimu hii inalenga kuwajengea abiria ujasiri wa kukataa na kuripoti vitendo vya ukatili wa kijinsia, huku ikisisitiza wajibu wa kila mmoja kulinda usalama na heshima ya wengine safarini.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀