𝐌𝐖𝐈𝐍𝐘𝐈; 𝐒𝐈𝐍𝐀 𝐍𝐈𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐎𝐍𝐆𝐄𝐙𝐀 𝐌𝐃𝐀 𝐖𝐀 𝐔𝐑𝐀𝐈𝐒


Dkt. Mwinyi ametoa kauli hiyo leo, Mei 23, 2026, alipofungua Jukwaa la Wenyeviti na Wakuu wa Taasisi za Umma katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, Airport, Mkoani Mkoa wa Mjini Magharibi.
Alieleza kuwa viongozi walioapa kulinda Katiba wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi, na kubainisha kuwa kipindi kilichobaki cha uongozi wake kitalenga utekelezaji mkubwa wa miradi ya maendeleo na sio mijadala isiyo na tija.
Mashirika ya Umma Kupunguziwa Ruzuku
Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Mwinyi ametoa onyo kali kwa mashirika ya umma yanayoendelea kutegemea ruzuku na mishahara kutoka serikalini badala ya kujiendesha kwa tija na faida.
"Serikali haitakuwa tayari kuendelea kubeba mzigo wa mashirika ya umma yanayotegemea ruzuku... Serikali itatoa muda mfupi kwa mashirika hayo kujipanga kujiendesha kwa faida, na yatakayoshindwa, serikali haitakuwa tayari kuendelea nayo," amesisitiza Rais Mwinyi.
Miradi ya Kimkakati na Dira ya 2050
Sambamba na hayo, Dkt. Mwinyi amesema serikali itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050 na kuimarisha miradi ya kimkakati ikiwemo:
- Maendeleo ya Bandari
- Viwanja vya Ndege
- Viwanja vya Michezo
- Miundombinu ya Barabara
kwa ujumla, Lengo kuu la miradi hii ni kuifanya Zanzibar kuwa kitovu cha uchumi endelevu na wa kisasa. Alihitimisha kwa kuwataka wenyeviti na watendaji wote wa taasisi hizo kutumia vizuri fursa zilizopo nchini ili kuongeza mapato na ufanisi.

Maoni
Chapisha Maoni