𝐖𝐀𝐒𝐈𝐎𝐉𝐔𝐋𝐈𝐊𝐀𝐍𝐀 𝐖𝐀𝐌𝐂𝐇𝐎𝐌𝐀 𝐌𝐎𝐓𝐎 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐌𝐊𝐄
Jeshi la Polisi nchini Kenya limesema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa shambulio la kuchomwa moto kwa mwanamke aliyesambaa mitandaoni baada ya kuchora tattoo ya Rais William Ruto pamoja na kauli za kisiasa mwilini mwake huwenda lilihusishwa na msimamo wa kisiasa.
Kwa mujibu wa Polisi, mwanamke huyo alivamiwa na watu wasiojulikana katika eneo la Mwiki jijini Nairobi na kumwagiwa petroli kabla ya kuwashwa moto, tukio lililomuacha na majeraha ya moto yanayokadiriwa kufikia asilimia 70 ya mwili wake.
Awali alipelekwa katika Hospitali ya Uzima Uhai kabla ya kuhamishiwa Kenyatta National Hospital kwa ajili ya matibabu maalum huku uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.
Kwa ujumla, Jeshi la Polisi nchini Kenya linaendelea na uchunguzi wa kuwabaini waliohusika na tukio hilo huku wananchi wakitaka haki ichukuliwe dhidi ya wahusika

Maoni
Chapisha Maoni