𝐌𝐔𝐅𝐓𝐈 𝐌𝐊𝐔𝐔 𝐓𝐙: 𝐒𝐈𝐊𝐔𝐊𝐔𝐔 𝐘𝐀 𝐄𝐈𝐃 𝐀𝐋-𝐀𝐃𝐇𝐀 𝐍𝐈 𝐉𝐔𝐌𝐀𝐓𝐀𝐍𝐎, 𝐌𝐄𝐈 27

 
Na, Thadeo Gelema 

Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Bin Zuber Ally, amewatangazia Waislamu na wananchi wote kwa ujumla kuwa Sikukuu ya Eid Al-Adha mwaka huu itakuwa siku ya Jumatano, Mei 27, 2026.

​Ujumbe Kutoka Makkah

​Akiongea akiwa nchini Saudi Arabia katika mji mtukufu wa Makkah, Sheikh Zubeir amewaombea heri waumini waliopo kwenye ibada ya Hijja na wale waliobaki nyumbani:

​ "Namuomba Mungu atukamilishie Hijja yetu, tupate Hijja iliyokamilika na wale wenzetu ambao hawakupata bahati ya kuja katika mawanja haya, waweze kutekeleza Ibada nyingine nyumbani na Mungu awalete mwaka ujao hapa katika mawanja ya Makkah."

​Sherehe za Kitaifa Kufanyika Dar es Salaam

​Kwa mujibu wa taarifa iliyoripotiwa na Millard Ayo, Sherehe za Eid Al-Adha Kitaifa kwa mwaka huu zitafanyika mkoani Dar es Salaam.

​Swala ya Eid itasaliwa katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI BAKWATA Makao Mkuu, uliopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 1:30 asubuhi na kufuatiwa na Baraza la Eid mara tu baada ya kukamilika kwa Swala.

Kwa ujumla, kutangazwa rasmi kwa Eid Al-Adha kufanyika Mei 27 kunatoa fursa kwa Waislamu nchini kujiandaa na ibada ya uchinjaji, huku Dar es Salaam ikiwa kitovu cha sherehe hizi kitaifa mwaka huu


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀