UJUMBE WA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KUTOKA KWA RAIS WA KIMATAIFA

 

Leo March 08, 2026 Rais wa Kimataifa wa Standup for Women Society (SWS), Deborah A. Ijadele-Adetona, ametoa wito kwa wanawake duniani kuendelea kushirikiana, kuinuana na kuwekeza kwa wenzao ili kuleta maendeleo ya jamii.

Akitoa ujumbe wake International Women’s Day, amesema siku hiio ni fursa ya kutambua mchango mkubwa wa wanawake katika kujenga familia, jamii na mataifa, pamoja na kuthamini jitihada za wale waliovunja vikwazo na kuendelea kupigania haki na maendeleo ya wanawake.

Amesema kaulimbiu ya mwaka huu “Give to Gain” (Toa ili Upate) inasisitiza umuhimu wa kusaidiana, kufundishana na kuunda fursa kwa wanawake na wasichana ili kuimarisha maendeleo jumuishi katika jamii.

Ameongeza kuwa SWS itaendelea kuhamasisha uwezeshaji wa wanawake, kukuza uongozi jumuishi unaozingatia usawa wa kijinsia na kujenga utamaduni wa mshikamano miongoni mwa wanawake duniani.

Kwa ujumla, Katika ujumbe wake, amewahimiza wanawake kusimama imara katika malengo yao, kuamini katika uwezo wao na kuendelea kuwainua wanawake wengine ili kujenga dunia yenye fursa sawa kwa kila mwanamke na msichana.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀