TUMIA IPASAVYO ALAMA YA PEMBETATU

 

Picha: Sajenti David Ndimila akiwafundisha madereva juu ya matumizi sahihi ya alama ya pembetatu kuzuia aja





Leo March 01, 2026  Madereva wa magari ya kubeba abiria wamekumbushwa umuhimu wa kubeba na kutumia ipasavyo alama ya pembetatu ya tahadhari (reflective triangle) pindi gari linapopata hitilafu barabarani, ili kuzuia ajali na kulinda usalama wa watumiaji wengine wa barabara.

Akizungumza na madereva hao, Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga, Sajenti David Ndimila, amesema alama hiyo ni muhimu kwa kuwaonya madereva wengine kuhusu uwepo wa gari lililoharibika, ajali au hatari iliyo mbele yao.

Ameeleza kuwa alama ya pembetatu inapaswa kuwekwa nyuma ya gari lililopata hitilafu na wakati mwingine mbele, kulingana na mazingira ya barabara, ili ionekane kwa urahisi mchana na usiku.

Kwa mujibu wa Sajenti Ndimila, alama hiyo inatakiwa kuwekwa umbali wa mita 50 hadi 100 kutoka lilipo gari lililoharibika. Umbali wa mita 100 unapendekezwa katika barabara za mwendo kasi, huku mita 50 zikitumika katika barabara za mijini au maeneo yenye mwendo wa chini.

Kwa Ujumla, Amesisitiza kuwa uzingatiaji wa taratibu hizi ni hatua muhimu katika kupunguza ajali na kuimarisha usalama barabarani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀