Mwl. Moris Daudi Afunga Kampeni Chuoni STJOSO: “Nitaanza na Haya”

 


Na, Mwandishi wetu Chuoni 

Leo, mgombea wa nafasi ya urais wa serikali ya wanafunzi wa ST. Joseph College (STJOSO) 2026/2027, Mwl. Moris Daudi, amefunga rasmi kampeni zake chuoni, akibeba kaulimbiu yake ya “Mabadiliko Chanya ni Sasa”. Katika hotuba yake ya kufunga kampeni, Moris aliwahakikishia wanafunzi kwamba endapo atachaguliwa, ataanza na haya:

Nitaanza na haya:

Kuboresha computer lab na studio ya uandishi wa habari ili kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunzia.

Kuimarisha huduma ya Wi-Fi chuoni, ili intaneti iwe ya haraka, thabiti na inafaa kwa masomo na utafiti.

Kuangalia upya na kuboresha utaratibu wa tisheti za Jumatano na Ijumaa, kuhakikisha ubora unaowiana na mahitaji ya wanafunzi.

Kuboresha mazingira ya hosteli kuwa salama, safi na rafiki – jambo ambalo bado linahitaji tathmini ya moja kwa moja.

Kushughulikia changamoto za kiusafiri, kuhakikisha usafiri wa wanafunzi ni salama, wa haraka na unalingana na ratiba ya masomo.”

Kwa upande wake, mgombea mwenza wa nafasi ya Makamu wa Rais, Maria Baraza, ameeleza kuwa atakazia zaidi mazingira bora ya hosteli, huduma za masomo, na usalama wa wanafunzi, akisisitiza kwamba maendeleo ya mwanafunzi yanahitaji kuanza na mazingira salama, rafiki na yenye kukidhi mahitaji muhimu.

Picha: Mbali mbali  AKIWA na timu yake huku wakiguatilia changamoto Kwa ukalibu









Mwl. Moris, anayejulikana kwa umaarufu wake wa michezo, ucheshi, moyo wa kujitolea na urafiki, amesema timu yake tayari imeweza kutembelea sehemu zenye changamoto chuoni, ikiwa ni pamoja na computer lab na studio ya uandishi, ili kuona hali halisi ya changamoto za wanafunzi. Hata hivyo, kura zenu ni Mhimu 

Uchaguzi wa STJOSO 2026/2027 unatarajiwa kufanyika kesho, Machi 25, 2026, ambapo wanafunzi wote watapata nafasi ya kuchagua viongozi wao wapya wa serikali ya wanafunzi. Uzinduzi na kufunga kampeni za Moris Daudi zimeonesha kuanza kwa ushindani mkali, huku kaulimbiu yake ya  Mabadiliko Chanya ni Sasa”.  matumaini ya maboresho dhahiri katika maisha ya wanafunzi chuoni.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀