MSIVUKE BARABARA MUONAPO MAGARI YA DHARURA YAKIPITA

Picha: Sajenti David Ndimila akitoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Nhelegani, Shinyanga

Hii ni Thadeo Media

Leo March 03, 2026 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nhelegani iliyopo mkoani Shinyanga wamepatiwa elimu ya usalama barabarani ili kuepuka kuvuka barabara wanapoona magari ya dharura yakipita.

Akitoa elimu hiyo, askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Shinyanga, Sajenti David Ndimila, amesema kuwa magari ya dharura ni yale yanayotoa huduma za kuokoa maisha na kulinda usalama wa umma. Magari hayo ni pamoja na ya kubebea wagonjwa, zimamoto na polisi.

Amefafanua kuwa magari ya dharura hupaswa kuwa na ving’ora au taa za bluu na nyekundu zinazomulika ili yapatiwe kipaumbele barabarani.

Aidha, Sajenti Ndimila amewasisitiza wanafunzi hao kuongeza umakini wanapotaka kuvuka barabara. Hata wanapokuwa kwenye kivuko cha watembea kwa miguu, wanapaswa kutoa kipaumbele kwa magari ya dharura kupita kwanza.

Picha: Sajenti David Ndimila akitoa elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Nhelegani mkoani Shinyanga kuhusu umuhimu wa kutovuka barabara wakati magari ya dharura yanapopita.


Kwa ujumla, Wanafunzi wametakiwa kutovuka barabara magari ya dharura yanapopita ili kulinda maisha yao na kutoa kipaumbele kwa huduma za uokoaji.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀