CHUKUENI TAHADHARI MNAPOKIMBIA MCHAKAMCHAKA BARABARANI

picha: Askari Polisi Koplo Zuhura Mlungwana akiwapa maelekezo ya usalama.

Hii ni Thadeo Media 

Leo Jumatano ya Februari 18, 2026 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyashimbi iliyopo Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga wamepatiwa elimu ya usalama barabarani Kwa kuchukua tahadhari pindi wawapo katika mazoezi ya mchakachaka barabarani.

Akitoa elimu hiyo Askari Polisi wa Kikosi Cha usalama barabarani Wilaya ya Kahama Koplo Zuhura Mlungwana amewaelimisha wanafunzi hao kujipanga upande wa kushoto wa barabara ikiwa ndio upande sahihi wa kukimbilia wakiwa katika mazoezi yao pamoja na kuwapanga washika vibendera mbele ya kundi na nyuma ili waweze kuongoza kundi hilo barabarani 

Koplo Zuhura amewasisitiza kujipanga mistari mitatu hadi minne wakati wa mazoezi ili kupunguza msongamano barabarani na kuepuka ajali pindi watakapo kanyagana na kuanguka.

Picha: Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyashimbi wakiwa kwenye mazoezi ya mchakachaka barabarani, wakiwa wamepangwa vizuri huku polisi akiwapa maelekezo ya usalama.

Kwa ujumla, Elimu ya usalama barabarani kwa wanafunzi wa Nyashimbi ni muhimu ili kuzuia ajali. Wanafunzi wanashauriwa kuzingatia mafunzo ya polisi na kushirikiana kuhakikisha mazoezi ya mchakachaka yanafanyika salama.

Maoni

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀