Habari
Kesi ya Jengo la Ghorofa Kariakoo: Wawili Waachiwa Huru, Hatima ya WashtakiwaWanne Yabaki Kitendawili
Wawili hao ambao ni Zenabu Silam (61) na Ashour Awadhi Ashour (38) wameachiwa huru leo baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) kusema hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi yao.
Hatua hiyo imekuja baada ya Wakili wa Serikali, Christopher Olembelle kumueleza Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mhini ya kwamba DPP amewasilisha hati ya kutoendelea na kesi dhidi ya washtakiwa hao wawili.
Washtakiwa wanne waliobaki katika kesi hiyo ni Leondela Mdete (49), Soster Nziku (55), Aloyce Sangawe (59) na Stephen Nziku (28) wote ni wakazi wa Dar es Salaam.
Washtakiwa wote wanadaiwa kutenda kosa hilo, Novemba 16, 2024 katika mtaa wa Mchikichi na Congo eneo la Kariakoo ambapo isivyo halali walishindwa kutimiza majukumu yao na kusababisha vifo vya watu 31.
Uamuzi wa Mahakama kuachia huru wawili katika kesi ya jengo la ghorofa Kariakoo unatoa taswira ya haki kisheria, huku washtakiwa wanne waliobaki wakikabiliwa na kesi nzito. Tukio hili linafunua changamoto za uwajibikaji wa majengo, usalama wa wananchi, na umuhimu wa mfumo wa kisheria kuhakikisha haki inatendeka kwa wote bila upendeleo.
Maoni
Chapisha Maoni