Habari

 Dkt. Mwinyi Aongoza Baraza la Mapinduzi na Kuapisha Mkuu wa Mkoa

Na Thadeo Media 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameongoza Kikao cha Kwanza cha Baraza la Mapinduzi (BLM) cha Kipindi cha Pili cha Serikali ya Awamu ya Nane.

Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 29 Disemba 2025, Ikulu, Zanzibar.

Kikao hicho cha BLM pia kimeambatana na uapisho, ambapo Rais Dkt. Mwinyi amemuapisha Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mhe. Mgeni Khatibu Yahya, aliyemteua hivi karibuni.

Kabla ya uteuzi huo, Mhe. Mgeni alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Chakechake, Pemba.

Kikao hiki kinaashiria mwanzo wa utekelezaji wa majukumu ya Serikali ya Awamu ya Nane katika Kipindi cha Pili, kikionesha dhamira ya kuimarisha utawala bora na kuwatumikia wananchi kwa ufanisi.






Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀