Magazeti
BALOZI DKT. NCHIMBI AZINDUA KAMPENI SHINYANGA MAJIMBO YA KISHAPU, SHINYANGA MJINI, SOLWA, ITWANGI RATIBA YA KESHO ISAKA NA KAHAMA
Shinyanga, Septemba 3, 2025 – Mgombea Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ameongoza mkutano mkubwa wa kampeni leo katika majimbo ya Kishapu na Shinyanga Mjini. Maelfu ya wananchi walihudhuria miutano hiyo, wakiwa tayari kusikia mpango wa chama kwa uchaguzi ujao.
Katika mkutano huo, Dkt. Nchimbi aliwahimiza wananchi kuendelea kuiunga mkono CCM na wagombea wake wa ubunge na udiwani. Wagombea walioahidiwa kuungwa mkono ni:
Mhe. Patrobas Katambi – Shinyanga Mjini
Mhe. Lucy Mayenga – Kishapu
Mhe. Ahmed Salum – Solwa
Mhe. Azza Hillal Hamad – Itwangi
Wabunge hao pia walizungumza kwa ufupi, wakieleza utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika majimbo yao, ikiwemo ujenzi wa barabara, masoko, shule, vituo vya afya, na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Ibadakuli.
Kwa mujibu wa ratiba ya kampeni iliyothibitishwa na Misalaba Media, ziara za CCM zitaendelea kesho Alhamisi, Septemba 4, 2025, katika maeneo ya Isaka na Kahama, ambapo viongozi na wagombea watakutana na wananchi kuendeleza kampeni.
Maoni
Chapisha Maoni