Siasa
Kura za Maoni CCM Kahama: Lukubha, Magangila na Cherehani Watingisha Majimbo ya Msalala, Kahama Mjini na Ushetu
Na Mwandishi Wetu – Kahama, Agosti 5
Katika mchakato wa kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kahama, Benjamin Lukubha Ngaiwa aliibuka mshindi kwa nafasi ya ubunge wa Jimbo la Kahama Mjini, baada ya kupata kura 2,093, akiwashinda wagombea wengine sita.
| Benjamin Lukubha Ngaiwa |
Aliyeshika nafasi ya pili alikuwa Sweetbert Charles Nkuba aliyepata kura 1,389, akifuatiwa na Jumanne Kibela Kishimba aliyepata kura 1,144. Wengine waliopata kura ni:
Francis Fikili Mihayo – kura 821
Juliana Kajala Pallangyo – kura 256
James Daudi Lembeli – kura 219
David Anyandwile Kilala – kura 191
Kwa upande wa Jimbo la Msalala, jumla ya kura 7,845 zilipigwa ambapo kura 7,685 zilikuwa halali na 160 ziliharibika. Katika matokeo hayo, Mabula J. Magangila aliongoza kwa kura 5,518, akifuatiwa na:
| Mabula J. Magangila |
Ambrose N. Nakale – kura 929
Ezekiel Maige – kura 791
Simon James Lufega – kura 189
Edson Simba Masondole – kura 152
Ramadhani Shiganza – kura 105
Wakati huo huo, katika Jimbo la Ushetu, CCM Wilaya ya Kahama ilimtangaza Emmanuel Peter Cherehani kuongoza katika matokeo ya awali, akipata kura 5,656. Hata hivyo, matokeo ya mwisho yalikuwa yakisubiriwa kutokana na marudio ya uchaguzi katika kata za Ubagwe, Mapamba na Bulungwa kufuatia malalamiko ya baadhi ya wanachama.
| Emmanuel Peter Cherehani |
Wagombea wengine katika jimbo hilo walipata kura zifuatazo:
Valelia Wilson Mwampashe – kura 153
Machibya Mwambilija Dofu – kura 171
Mussa Shilanga Misungwi – kura 452
Katibu wa CCM Wilaya ya Kahama, Andrew Chatwanga, aliwataka wanachama wote na wagombea kuwa watulivu, wakisubiri kwa subira na nidhamu maamuzi ya vikao vya juu vya chama, akisisitiza kuwa CCM inaongozwa na misingi ya haki, ustaarabu na maadili.
Kwa taarifa zaidi za kisiasa na maendeleo ya uchaguzi ndani ya CCM, tembelea daima Thadeo Media
Maoni
Chapisha Maoni