Siasa

 Ahmed Salum Aliongoza Kura za Maoni CCM Jimbo la Solwa

Na Mwandishi Wetu – Thadeo Gelema, Agosti 5

Mbunge wa zamani wa Jimbo la Solwa, Ahmed Ally Salum, aliongoza kwa kishindo kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizofanyika tarehe 4 Agosti 2025 katika Wilaya ya Shinyanga Vijijini.

Katika kura hizo, Salum alipata kura 3,862 kati ya kura halali 7,012 zilizopigwa, huku hakuna kura iliyoharibika. Aliongoza kwa tofauti kubwa dhidi ya wagombea wengine sita waliokuwa wakichuana naye kwenye mchakato huo wa ndani ya chama.

Aliyeshika nafasi ya pili alikuwa Sosthenes Julius Katwale aliyepata kura 2,288. Wengine waliopata kura ni Selemani Emmanuel Chokala (645), Zinguji Mayala Machwele (67), Alphistone Michael Bushi (61), Costantine Joseph Budaga (59), na Leonard Nduta Lukanya aliyepata kura 30 pekee.

Matokeo hayo yalitangazwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Shinyanga Vijijini ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi, Bi Erenestina Richard. Hata hivyo, alifafanua kuwa ushindi huo si uteuzi rasmi wa mgombea.

 “Haya ni matokeo ya awali ya kura za maoni. Kuongoza hapa hakumaanishi tayari umeteuliwa. Tunawaomba wagombea wote kuwa watulivu wakisubiri uamuzi wa vikao vya juu vya chama,” alisema Erenestina.

Wanachama wa CCM waliojitokeza kushiriki kura hizo walionesha hamasa kubwa, jambo linalodhihirisha nguvu ya demokrasia ya ndani ya chama kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Endelea kufuatilia Thadeo Media kwa taarifa zaidi 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆 𝐍𝐄𝐖𝐒: 𝐌𝐇𝐄. 𝐃𝐊𝐓. 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐀𝐌𝐄𝐅𝐀𝐍𝐘𝐀 𝐔𝐓𝐄𝐔𝐙𝐈

BREAKING: RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

𝐓𝐀𝐇𝐀𝐃𝐇𝐀𝐑𝐈: 𝐏𝐎𝐋𝐈𝐒𝐈 𝐖𝐀𝐊𝐀𝐍𝐔𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐕𝐔𝐌𝐈 𝐌𝐖𝐀𝐍𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐈 𝐔𝐃𝐎𝐌 𝐊𝐔𝐖𝐀𝐖𝐀