Maisha ya chuoni
PICHA: MAPUMZIKO YA MTIHANI – WANAFUNZI WAKIJIANDAA NA MTIHANI WA MCHANA ST. JOSEPH’S COLLEGE
St. Joseph’s College – Shinyanga
Jumatatu, 28 Julai 2025
Siku ya kwanza ya mitihani ya mwezi Julai chuoni St. Joseph’s College Shinyanga imeanza rasmi leo asubuhi kuanzia saa 2:00. Baada ya mtihani wa awali, wanafunzi walipata mapumziko mafupi kabla ya kuendelea na mtihani wa mchana unaoanza saa 6:00.
Katika muda huo wa mapumziko, wanafunzi wameonekana wakijisomea, kujadiliana na kutafakari mada mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea mtihani wa mchana. Sehemu mbalimbali za chuo zilijaa utulivu huku mazingira yakibeba hali ya kujiandaa kwa bidii na umakini hasa.
Mitihani hii imepangwa kuendelea hadi Ijumaa, Agosti 1, 2025, kwa ratiba maalum iliyotolewa mapema wiki iliyopita.
Maoni
Chapisha Maoni