PIGO KWA KANISA KATOLIKI: KARDINALI PENGO AFARIKI
Na, Thadeo Gelema
Kanisa Katoliki nchini Tanzania limeingia katika maombolezo kufuatia kifo cha Mhashamu Kardinali Polycarp Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo Februari 19, 2026 majira ya saa 4:00 akiwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu
Taarifa rasmi kutoka Jimbo Kuu la Dar es Salaam imethibitisha kifo hicho na kueleza kuwa taratibu na ratiba za mazishi zitatolewa baadaye baada ya mipango kukamilika. Kardinali Pengo alikuwa mmoja wa viongozi wakuu wa Kanisa Katoliki waliotoa mchango mkubwa katika kuimarisha imani, maadili, amani na mshikamano wa kitaifa. Katika kipindi chote cha utumishi wake, alijulikana kwa sauti yake ya busara katika masuala ya kijamii, kiroho na kitaifa, jambo lililompa heshima kubwa ndani na nje ya nchi
Kwa ujumla, Kifo cha Kardinali Pengo ni pengo kubwa kwa Kanisa na Taifa kwa ujumla. Ataendelea kukumbukwa kwa uongozi wake uliotukuka na huduma yake kwa Mungu na jamii.
*Bwana ampe pumziko la milele.*
😭😭😭
JibuFuta