VIJANA SHINYANGA TUMIENI FURSA ZA KIUCHUMI KUJIKWAMUA
Na Mwandishi Wetu, Shinyanga Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka, amewataka vijana wa Mkoa wa Shinyanga kuacha kuwa watazamaji wa masuala ya kiuchumi na badala yake wawe washiriki wakuu katika kuleta maendeleo ya mkoa na taifa. Akizungumza Februari 21, 2026 wakati wa uzinduzi wa Jukwaa la Vijana mkoani humo, Nanauka amesema Serikali imeweka mazingira rafiki kwa vijana kupitia mikopo, mafunzo ya ujuzi na matumizi ya teknolojia ili kuwawezesha kujiajiri na kukuza biashara. Amesisitiza kuwa vijana wana nafasi kubwa ya kuanzisha viwanda vidogo, kujenga mitandao ya biashara na kuongeza thamani ya rasilimali zilizopo. Aidha, amebainisha kuwa tayari mikataba zaidi ya saba imeingiwa kwa ajili ya kuwapeleka vijana kufanya kazi nje ya nchi, huku shilingi bilioni 200 zilizotolewa na Rais zikianza kutumika kuwawezesha vijana kiuchumi. Katika mwaka wa fedha 2024/2025, zaidi ya shilingi bilioni 2 zimetolewa kupitia mikopo ya asilimia 10 mkoani Shinyanga, pamoja na ...