ZIARA YA MAADILI YA KIUTU ILIFANA ST. JOSEPH'S COLLEGE – WAHITIMU WALIJIFUNZA KWA VITENDO KUGUSA MAISHA. Bushushu – Shinyanga Society Offers Taarifa rasmi: Jumapili, 27 Julai 2025 Katika kuendeleza maadili ya utu, huruma na mshikamano wa kijamii, wanafunzi wa St. Joseph’s College – Shinyanga wamehitimisha kwa mafanikio ziara ya kipekee ya kuwatembelea watoto wenye mahitaji maalum katika kituo cha Shinyanga Society Offers – Bushushu. Ziara hiyo iliyofanyika jana, Jumamosi, Julai 26, iliwakutanisha wanafunzi, viongozi wa serikali ya wanafunzi na walimu walezi katika safari ya kiroho yenye kugusa mioyo na kubadili mitazamo. Wakiwa kituoni, wanafunzi walishiriki shughuli mbalimbali ikiwemo: SHUGHULI WALIZOFANYA: Kukabidhi misaada ya kijamii (sabuni, vifaa vya shule, na fedha) Kuzungumza na watoto na walezi wao Kujifunza changamoto za maisha ya wenye mahitaji maalum Kutoa neno la faraja, upendo na tumaini kama “Kuwahudumia waliopuuzwa si ukarimu wa muda mfupi, bali ni...