KAULI ZA WATU WASIO NA MALENGO KATIKA KAZI / BIASHARA
Imeandaliwa na: Up-line: Thadeo Gelema, Thadeo Media Katika dunia ya kazi na biashara, mafanikio huanza na mtazamo wa mtu. Watu wengi hushindwa si kwa sababu hawana uwezo, bali kwa sababu ya kauli wanazojenga akilini mwao. Kauli hizi hugeuka kuwa vizuizi vinavyokwamisha maendeleo yao kila siku. Kauli Zinazowarudisha Nyuma Wengi “ Sina mtaji” Mtaji si fedha pekee. Ujuzi, muda, nguvu na mtandao wa watu ni rasilimali tosha kuanza hatua ndogo. Wengi waliofanikiwa walianza na walichokuwa nacho. “ Nitaanza lazima kesho” Kesho isiyofika ndiyo adui wa mafanikio. Kila mafanikio huanza na hatua ya leo, hata kama ni ndogo. “ Sina mawasiliano” Mahusiano hujengwa. Kushiriki kwenye matukio, kutumia mitandao ya kijamii vizuri na kujitambulisha kwa watu hufungua milango ya fursa. “ Mimi ni wa hivi hivi tu” Hii ni kauli ya kujidharau. Ukuaji wa mtu hutegemea namna anavyojiona. “ Ndugu zangu wamenitenga” Mafanikio ni jukumu binafsi. Wengi waliofanikiwa walianza bila msaada wa karibu. “ Sina bahati” Baha...